عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَقَفَ عَلَى نَاسٍ جُلُوسٍ، فَقَالَ:
«أَلاَ أُخْبِرُكُمْ بِخَيْرِكُمْ مِنْ شَرِّكُمْ؟» قَالَ: فَسَكَتُوا، فَقَالَ ذَلِكَ ثَلاَثَ مَرَّاتٍ، فَقَالَ رَجُلٌ: بَلَى يَا رَسُولَ اللهِ، أَخْبِرْنَا بِخَيْرِنَا مِنْ شَرِّنَا، قَالَ: «خَيْرُكُمْ مَنْ يُرْجَى خَيْرُهُ وَيُؤْمَنُ شَرُّهُ، وَشَرُّكُمْ مَنْ لاَ يُرْجَى خَيْرُهُ وَلاَ يُؤْمَنُ شَرُّهُ».
[صحيح] - [رواه الترمذي] - [سنن الترمذي: 2263]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alisimama kwa watu waliokaa, akasema:
"Je, nisikuelezeni mbora wenu na muovu wenu?" Anasema: Wakanyamaza, akalisema hilo mara tatu, mtu mmoja akasema: Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tueleze mbora wetu na muovu wetu, akasema: "Mbora wenu ni yule inayetarajiwa heri yake, na kuaminiwa kutokuwepo kwa shari yake, na muovu wenu ni yule isiyetarajiwa heri yake, na kutoaminiwa shari yake".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy] - [سنن الترمذي - 2263]
Alisimama Mtume rehema na amani ziwe juu yake mbele za watu waliokaa miongoni mwa Maswahaba zake akawauliza, je nisikuelezeni na nikumbusheni ni nani mbora wenu na ni nani muovu wenu? Wote hawakuzungumza na wala hawakujibu chochote, kwa kuhofia kubainishwa mbora wao na muovu wao na wakahofia fedheha wakanyamaza. Mtume rehema na amani ziwe juu yake akarudia swali mara tatu, akajibu mtu mmoja miongoni mwao: Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tueleze mbora wetu na muovu wetu. Mtume rehema na amani ziwe juu yake akawabainishia: Kuwa mbora wenu ni yule inayesubiriwa na kutarajiwa heri yake na ihisani yake na wema wake, na kuaminiwa kutowepo shari yake kusiogopwe uadui wake na uonevu wake na dhuluma yake, na kuwa muovu wenu ni yule asiyetarajiwa wala kusubiriwa wala kutamaniwa kupatikana heri yake na ihisani yake na wema wake, na haiaminiwi shari yake, bali unahofiwa uadui wake na uonevu wake na dhuluma yake.