عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال:

لأن أحلف بالله كاذبًا أحب إليَّ من أن أحلف بغيره صادقًا.
[صحيح] - [رواه ابن أبي شيبة وعبد الرزاق، لكن عبد الرزاق على الشك في ابن مسعود أو ابن عمر]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "kuapa kwangu kwa jina la Mwenyezi Mungu kwa uongo napenda zaidi kuliko kuapa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu nikisema ukweli".
Sahihi - Imepokelewa na Ibn Abii Shaybah

Ufafanuzi

Anasema bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Kuapa kwangu kwa jina la Mwenyezi Mungu juu ya kitu ambacho mimi ninasema uongo -tukichukulia kutokea hilo- kunapendeka zaidi kwangu kuliko kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu juu ya kitu ambacho mimi ni mkweli ndani yake; na hii nikuwa kuapa kwa Mwenyezi Mungu kwa uongo kumeshinda kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu kwa ukweli; kwasababu kuapa kwa Mwenyezi Mungu katika hali hii kuna uzuri wa tauhidi, na kuna ubaya wa dhambi la uongo, na kuapa kwa asiyekuwa yeye kwa ukweli, kuna uzuri wa ukweli na dhambi ya ushirikina, na zuri la tauhidi ni kubwa zaidi kuliko zuri la ukweli, na dhambi la uongo ni jepesi sana kuliko dhambi la ushirikina.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno

Ziada