عَنْ ثَابِتَ بْنَ الضَّحَّاكِ رضي الله عنه، وَكَانَ مِنْ أَصْحَابِ الشَّجَرَةِ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:

«مَنْ حَلَفَ عَلَى مِلَّةٍ غَيْرِ الإِسْلاَمِ فَهُوَ كَمَا قَالَ، وَلَيْسَ عَلَى ابْنِ آدَمَ نَذْرٌ فِيمَا لاَ يَمْلِكُ، وَمَنْ قَتَلَ نَفْسَهُ بِشَيْءٍ فِي الدُّنْيَا عُذِّبَ بِهِ يَوْمَ القِيَامَةِ، وَمَنْ لَعَنَ مُؤْمِنًا فَهُوَ كَقَتْلِهِ، وَمَنْ قَذَفَ مُؤْمِنًا بِكُفْرٍ فَهُوَ كَقَتْلِهِ»، هَذَا لفْظُ البُخَارِيِّ، وَلِمُسْلِمٍ: «وَمَنْ ادَّعَى دَعْوَى كَاذِبَةً لِيَتَكَثَّرَ بِهَا لَمْ يَزِدْهُ اللهُ إِلَّا قِلَّةً».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Thabit bin Dhwahaki- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba yeye alimuunga mkono Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- chini ya mti, nakuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakaye apa juu ya kiapo cha mila isiyokuwa ya uislamu kwa uongo tena kwa makusudi basi atakuwa kama alivyosema, na atakayeua nafsi kwa kitu chochote ataadhibiwa nacho siku ya kiyama, na hakuna uwajibu juu ya mtu ya kuweka nadhiri katika vile asivyovimiliki" Na katika riwaya nyingine: "Na kumlaani muumini ni sawa na kumuuwa". Na katika riwaya: "Na atakayedai madai ya uongo ili ajichumie (mali) kupitia madai hayo hatomzidishia Mwenyezi Mungu -Mtukufu- isipokuwa upungufu".

الملاحظة
وَلِمُسْلِمٍ: «وَمَنْ ادَّعَى دَعْوَى كَاذِبَةً لِيَتَكَثَّرَ بِهَا لَمْ يَزِدْهُ اللهُ إِلَّا قِلَّةً يجعل مفردا ولا يكون مع هذا الحديث
النص المقترح لا يوجد...
الملاحظة
رواية مسلم تكون في حديث مستقل، وسيتم الشرح بناء عليه
النص المقترح لا يوجد...

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Amepokea Thabit bin Dhwahaki Al-Answariy -mmoja kati ya waliomuunga mkono Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- chini ya mti, katika mkataba wa maridhiano siku ya vita vya hudaibia, kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye amesema katika maana ya maneno yake: Atakaye apa juu ya kiapo kilicho nje ya sheria ya uislamu, mfano akasema: Yeye ni Myahudi au mkristo, au yeye ni majusi, au yeye ni kafiri au kajitenga mbali na Mwenyezi Mungu na Mtume wake itakapokuwa kadhaa wa kadhaa, akadhamiria kusema uongo katika kiapo chake basi atakuwa kama alivyojinasibishia katika moja miongoni mwa mila za kikafiri. Na atakayeiuwa nafsi yake kwa kitu chochote, kama panga, au kisu, au risasi, au kinginecho katika vifaa vya kuulia, ataadhibiwa nacho siku ya kiyama. Na atakayetia nadhiri ya kitu ambacho hakimiliki kama akiweka nadhiri ya kumuacha huru mtumwa wa fulani, au kutoa sadaka katika mali ya fulani, basi nadhiri yake imeharibika na wala haizingatiwi; kwasababu haijaangukia mahala pake, na haijashuka mahala pake. Na atakayemlaani muumini, atakuwa ni kama kamuuwa, kwa kushirikiana mtoa laana na muuwaji kuvunja maharamisho ya Mwenyezi Mungu- Mtukufu- na kuchuma madhambi, na kustahiki adhabu. Na atakayekua na kiburi na akataka wingi wa mali kwa kuleta madai ya uongo yasiyokuwepo, katika mali au elimu au nasaba au utukufu au cheo au kinginecho, akitaka kwa hilo kuongezeka, hatomzidishia Mwenyezi Mungu isipokuwa udhalili na unyonge; kwasababu yeye ametaka kuinyanyua nafsi yake kwa yasiyokuwepo, hivyo malipo yake yataendana na namna ya makusudio yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kireno Kimalayo
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno