عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:

«وَيْلٌ لِلْأَعْقَابِ مِنَ النَّارِ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira na Abdillahi bin Amri na Aisha- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye amesema: (Adhabu kali ya moto itazipata nyayo za miguu).
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anatahadharisha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- juu ya kufanya uzembe katika swala la udhu, na kutotekeleza udhu vilivyo, na anahimiza juu ya kuzingatia kuukamilisha, na kwakuwa mwisho wa miguu mara nyingi ndio huwa hayafiki maji ya udhu, basi mapungufu yanakuwa katika twahara na swala kwasababu hiyo, na akaeleza kuwa adhabu itamiminika juu ya hilo na kwa mfanyaji wake anayefanya uzembe katika twahara yake ya kisheria.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno

ويل:
كلمة وعيد وتخويف وتهديد.