«لَا يَزَالُ يُسْتَجَابُ لِلْعَبْدِ مَا لَمْ يَدْعُ بِإِثْمٍ أَوْ قَطِيعَةِ رَحِمٍ، مَا لَمْ يَسْتَعْجِلْ» قِيلَ: يَا رَسُولَ اللهِ مَا الِاسْتِعْجَالُ؟ قَالَ: يَقُولُ: «قَدْ دَعَوْتُ وَقَدْ دَعَوْتُ، فَلَمْ أَرَ يَسْتَجِيبُ لِي، فَيَسْتَحْسِرُ عِنْدَ ذَلِكَ وَيَدَعُ الدُّعَاءَ».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2735]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- hadithi Marfu'u: "Hujibiwa mmoja wenu anapokuwa hajafanya haraka: anasema: Nimemuomba Mola wangu, na wala sijaona ananijibu mimi" Na katika riwaya ya Muslim: "Hatoacha kuendelea kujibiwa mja madam tu hajaomba dhambi, au kukata ukoo na madam hajafanya haraka" pakasemwa: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kufanya haraka? akasema: "Anasema: Nimeomba, hakika nimeomba, wala sijaona ananijibu, akakata tamaa na wakati huo akaacha kuomba".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]
Anaeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwamba hujibiwa mja dua zake madam tu hajaomba kutenda maasi au kukata ukoo, na madam hajafanya haraka, pakasemwa: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kufanya haraka kunakoambatana na kuzuiliwa kujibiwa dua?, akasema: ni mtu kusema: Hakika nimeomba, na nimeomba, na nimerudia rudia kuomba, lakini hajanijibu; akafanya haraka wakati huo na akaacha kuomba.