«إِنَّهُ لَيَأْتِي الرَّجُلُ العَظِيمُ السَّمِينُ يَوْمَ القِيَامَةِ لاَ يَزِنُ عِنْدَ اللَّهِ جَنَاحَ بَعُوضَةٍ، وَقَالَ: اقْرَؤُوا، {فَلاَ نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ القِيَامَةِ وَزْنًا} [الكهف: 105]».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 4729]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hakika atakuja mtu mnene tena mkubwa siku ya kiyama akiwa halingani mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]
Hakika mtu mkubwa ni yule mwenye nia kubwa mwenye kujikweza kwa waja wa Mwenyezi Mungu duniani mwenye kujipa ujabari mwenye kujifaharisha kwa matendo yake na kauli zake, basi huyo siku ya kiyama hatolingana mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu, na wala hatokuwa na thamani wala nafasi.