عن أنس بن مالك رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم:

«من قال -يعني: إذا خَرج من بَيتِه-: بِسم الله تَوَكَّلتُ على اللهِ، وَلاَ حول ولا قُوَّة إِلَّا بالله، يُقَال له: هُدِيتَ وَكُفِيتَ وَوُقِيتَ، وَتَنَحَّى عَنه الشَّيطَان». زاد أبو داود: «فيقول -يعني: الشيطان- لِشَيطان آخر: كَيف لَك بِرَجلٍ قَد هُدِيَ وكُفِيَ ووُقِيَ؟».
[ضعيف] - [رواه أبو داود والترمذي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas bin Maliki -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayesema: -Yaani: anapotoka nyumbani kwake-: Bismillaahi tawakkaltu a'la llaahi -kwa jina la Mwenyezi Mungu nimemtegemea Mwenyezi Mungu, Laa haulaa walaa quwwata illaa billaa- hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, huambiwa: Umeongozwa na umetoshelezwa na umekingwa, na shetani hujitenga mbali naye". Ameongeza Abuudaudi: "Basi husema: -yaani shetani-: kuwaambia mashetani wengine: utaweza vipi kwa mtu aliyeongozwa na akatoshelezwa na akakingwa?".

الملاحظة
والنسائي في السنن الكبرى 9917
النص المقترح لا يوجد...
الملاحظة
وروي بنحوه عند ابن ماجه رقم 3886
النص المقترح لا يوجد...

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Ameeleza Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa mtu atakapotoka nyumbani kwake na akasema: Bismillaahi -kwa jina la Mwenyezi Mungu-, Tawakkalu a'lallaahi -Nimemtegemea Mwenyezi Mungu-, Laa haulaa walaa quwwata illaa billaahi- hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, Malaika humuita Ewe mja wa Mwenyezi Mungu umeongozwa katika njia ya haki, na umetoshelezwa mahitajio yako, na umehifadhiwa dhidi ya maadui; basi shetani aliyewakilishwa kwake hujitenga mbali naye, na hapo husema shetani mwingine kumwambia shetani huyu: utawezaje kumpoteza mtu tayari kaongozwa, na katoshelezwa, na amekingwa na mashetani wote? kwasababu yeye amesema maneno haya basi wewe hutomuweza.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno