Aina:
عَنْ الْبَرَاءَ رضي الله عنه:

عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ كَانَ فِي سَفَرٍ فَصَلَّى الْعِشَاءَ الْآخِرَةَ فَقَرَأَ فِي إِحْدَى الرَّكْعَتَيْنِ بِـ التِّينِ وَالزَّيْتُونِ. وَفِي لَفْظٍ: فَمَا سَمِعْتُ أَحَدًا أَحْسَنَ صَوْتًا أَوْ قِرَاءَةً مِنْهُ.
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 7546]
المزيــد ...

Kutoka kwa Barraa bin A'zib -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- "Yakwamba Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa safarini, akaswali swala ya ishaa ya mwisho, akasoma katika moja ya rakaa mbili kwa sura ya wattin wazzaitun, sijawahi kumsikia yeyote mwenye sauti nzuri au kisomo kizuri zaidi yake".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

Ufafanuzi

Alisoma Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa sura ya wattin wazzaitun ndani ya rakaa ya kwanza katika swala ya ishaa; kwasababu yeye alikuwa safarini, na safari ni lazima izingatiwe kufanya wepesi (tahfifu) kwasababu ya shida na matatizo yake, na pamoja nakuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa msafiri, lakini hakuyaacha yale yanayochochea kupatikana kwa utulivu na kuhudhurisha moyo wakati wa kusikiliza Qur'ani, nako ni kupendezesha sauti katika kisomo cha swala.

Katika Faida za Hadithi

Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (18)
Aina tofauti
Ziada