Aina:
عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه:

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه يُحَدِّثُ عَنْ رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، أَنَّهُ قَامَ فِيهِمْ فَذَكَرَ لَهُمْ أَنَّ الْجِهَادَ فِي سَبِيلِ اللهِ، وَالْإِيمَانَ بِاللهِ أَفْضَلُ الْأَعْمَالِ، فَقَامَ رَجُلٌ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، أَرَأَيْتَ إِنْ قُتِلْتُ فِي سَبِيلِ اللهِ، تُكَفَّرُ عَنِّي خَطَايَايَ؟ فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «نَعَمْ، إِنْ قُتِلْتَ فِي سَبِيلِ اللهِ، وَأَنْتَ صَابِرٌ مُحْتَسِبٌ، مُقْبِلٌ غَيْرُ مُدْبِرٍ»، ثُمَّ قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «كَيْفَ قُلْتَ؟» قَالَ: أَرَأَيْتَ إِنْ قُتِلْتُ فِي سَبِيلِ اللهِ أَتُكَفَّرُ عَنِّي خَطَايَايَ؟ فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «نَعَمْ، وَأَنْتَ صَابِرٌ مُحْتَسِبٌ، مُقْبِلٌ غَيْرُ مُدْبِرٍ، إِلَّا الدَّيْنَ، فَإِنَّ جِبْرِيلَ عَلَيْهِ السَّلَامُ قَالَ لِي ذَلِكَ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Qatada Haritha bin Ribiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye alisimama kati yao, akawaeleza kuwa kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na kumwamini Mweyezi Mungu ndio matendo bora, akasimama bwana mmoja akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hivi unaonaje ikiwa nitauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu, je yatafutwa makosa yangu? Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kumwambia: "Ndiyo, ikiwa utauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu na wewe ukiwa ni mwenye subira na kutaraji malipo ukiwa mstari wa mbele pasi na kurudi nyuma" Kisha akasema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Umesema vipi?" Akasema: Hivi unaonaje ikiwa nitauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu, je yatafutwa makosa yangu? Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kumwambia: "Ndiyo, ikiwa utauwawa katika njia ya Mwenyezi Mungu na wewe ukiwa ni mwenye subira na kutaraji malipo ukiwa mstari wa mbele pasina kurudi nyuma, isipokuwa deni; kwani Jibrili ziwe juu yake Amani kanieleza hivyo mimi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Alisimama Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kati ya maswahaba kwaajili ya kuwahutubia, akawaeleza kuwa kupigana jihadi kwaajili ya kulinyanyua jina la Mwenyezi Mungu na kumuamini Mwenyezi Mungu ndiyo matendo bora, akasimama bwana mmoja akamuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Hivi unaonaje kama nitauwawa kwaajili ya kulinyanyua jina la Mwenyezi Mungu je nitasamehewa mimi madhambi yangu?, akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Ndiyo, lakini kwa sharti uwe umeuwawa ukiwa na subira na uvumilivu kwa yale yaliyokupata, ukitakasa nia kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, bila kukimbia kiwanja cha vita, kisha akakumbuka Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kitu, nacho ni deni, akakumbusha kuwa jihadi na shahada havifuti haki za wanadamu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama

Maana ya Maneno

Aina tofauti
Ziada